Thursday, October 3, 2013

magazeti leo alhamisi






Mashine za TRA zazua balaa.. Mbeya wagoma kuzinunua, vurugu zazuka.....!


Mabomu ya machozi yalipigwa ili kuzuia wafanyabiashara wasilete vurugu

Wafanyabiashara hao walichoma matairi ili kuwazuia polisi wasiweze kuwafikia
Na Kenneth Ngelesi
WAFANYABIASHARA mkoani Mbeya wamezua kizaazaa wakigoma kufungua maduka wakipinga agizo la Mamlaka ya Mapato nchini (TRA) linalowataka kununua mashine za kielektroniki kwa ajili ya kukatia risiti za wateja pindi wanapowauzia bidhaa.
Katika sokomoko hilo lililotokea jana na kusababisha taharuki kwa muda kadhaa, wafanyabiashara hao wanadai kuwa gharama za mashine zitolewe na serikali.(P.T)